Alhamisi, 23 Aprili 2015

Kuomba

KUJIFUNZA KUWA WAKRISTO WAOMBAJI –LUKA 11:1 “BWANA, TUFUNDISHE SISI KUSALI”
Mpendwa katika Kristo Yesu,
Baada ya kujifunza somo la Kufunga na Kuomba nimeombwa kuingia kwa undani kidogo kwa habari ya uombaji. Wengine wanasema hawajui kuomba. Wengine wanasema wanajua kuomba lakini kwa kiwango kidogo sana. Wengine wanasema uombaji wao ni dakika 3 au 5 au 10 maneno yanawaishia!  Wengine wanasema wanataka nguvu ya Roho Mtakatifu kwa ajili ya kuomba. Basi nakusihi fuatana nami tujifunze toka chini kabisa habari ya kuomba. Ukienda nami pamoja na kuamua kufanyia kazi mambo tutakayojifunza nakuhakikishia baada ya wiki 2 utaanza kuona matokeo tofauti katika uombaji wako. Roho Mtakatifu atakusaidia. Nyakati za nyuma nilikuwa siwezi kuingia kwenye maombi na kukaa katika uwepo wa Mungu kwa Zaidi ya dakika 20. Baada ya kujifunza kuomba (na bado naendelea kujifunza) nimekuja kujikuta saa moja kila napoingia kwenye maombi haitoshi hata kidogo. Nakumbuka miaka kadhaa nyuma niliingia katika maombi alfajiri. Kama baada ya dakika 20 nikawa nimemaliza kuomba kwa haraka zangu nikakimbilia kuanza kujiandaa kwa ajili ya kwenda kazini. Roho Mtakatifu akaniambia una mambo mengi ya kuomba lakini huna muda wa kukaa nami kwa utulivu kuomba. Una haraka na mambo yako kuliko kuomba. Nilijisikia vibaya sana. Nikamwambia Bwana wangu nisaidie. Kuanzia siku hiyo nikajipangia muda maalumu wa kutosha wa kuomba. Nimemuona Roho Mtakatifu akibadilisha maisha yangu ya kimwili na kiroho siku baada ya siku kwa kuwa nimedhamiria kuwa na ushirika naye anibadilishe kwa ajili ya kumtumikia yeye. Naendelea kujifunza siku baada ya siku.  Nami nikusihi ungana nami tujifunze jambo.
Mpendwa wangu nikuambie tu ukweli kwamba  Maombi ni ujuzi unaohitaji mazoezi ya kila siku. Hakuna ujuzi unaokaa kwa mtu pasipo mazoezi. Hata Roho Mtakatifu anasema kwa kinywa cha Mtume Paulo kwa habari ya utauwa kwamba  “..ujizoeze kupata utauwa” #1Tim 4:7. Kama kuna juhudi zozote tunaweza kuzifanya katika maisha yetu ya kimwili basi juhudi zenye matokeo mazuri ni pale tutakapofanya juhudi na mazoezi ya mambo ya kiroho. Si maandiko yanasema ‘Mtakatifu azidi kujitakasa’? Basi tujizoeze kujitakasa, tujizoeze kuomba, tujizoeze kufunga, tujizoeze kufanya kazi ya Mungu. Miili, na nafsi zetu zikizoea basi inakuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku.
Tusikae tusubiri muujiza wa jinsi ya kuwa waombaji wazuri ndugu zangu. Tusikae tusubiri muujiza wa kuwa walimu wazuri. Tusikae tusubiri muujiza wa kuwa Manabii wazuri. Tusikae tusubiri muujiza wa kuwa wainjilisti wazuri. Tusikae kusubiri muujiza wa kuwa wachungaji wazuri. Hakuna muujiza. Ukisikia wito wa Roho Mtakatifu inuka anza safari ya huo wito. Ni lazima tukae chini tufanye mazoezi haya ya kiroho. Na kwa kuwa Roho Mtakatifu mwenyewe ndiye anayetufundisha basi tukionyesha utayari huo atatufundisha nasi tutakuwa wazoefu na wenye kujaa nguvu na utaalamu katika maombi.
Fungu ambalo linabeba somo hili linalopatikana katika Luka 11:1 limebeba uzito usio wa kawaida. Wanafunzi wa Yesu wanamwambia ‘Bwana tufundishe sisi kusali’. Waliomba ombi hili maalumu si kwamba ndo ilikuwa siku ya kwanza au ya pili wamekutana na Bwana Yesu. Bali ilikuwa muda mrefu tu wakifanya kazi naye. Na ombi hili walilitoa maalumu baada ya kumuona Bwana Yesu akiomba. Ngoja nikusomeshe huu mstari mzima unavyosema ‘Ikawa alipokuwa mahali fulani akiomba, alipokwisha, mmoja katika wanafunzi wake alimwambia, Bwana, tufundishe sisi kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake’.
Ndugu yangu unaweza kujiuliza ni kipi mwanafunzi huyu aliona ni cha tofauti katika maombi ya Bwana Yesu? Unaweza kujiuliza hilo? Ni nini alikiona hasa hata akajiona wao hawajui kuomba? Yamkini aliyachunguza kwa undani sana maisha ya Bwana Yesu kila siku. Alikuwa hana muda wa kupumzika ovyo ovyo. Usiku atakesha kwenye maombi, asbh ataamka na uchovu hatasema ngoja nikapumzike bali ataendelea na kazi. Wakati ambapo wanafunzi watakuwa wamechoka yeye atajitenga nao ataenda kuomba. Hata nyakati zingine wakiwa katika kutembea kuelekea sehemu Fulani yeye katikati ya kutembea huko ataingia katika maombi. Utaona kwa kiwango gani wanafunzi waligundua maisha ya maombi jinsi alivyokuwa Bwana Yesu. Na kwa kuwa Kristo ni kipimo chetu, kanisa la leo haliwezi kuepuka kujifunza kutoka kwa Bwana Yesu kwa habari ya maisha ya maombi. Na Bwana Yesu alitoa ile wazungu wanaita ‘pattern’ ya maombi. Akatufundisha ile ambayo madhehebu mengi wanaiita SALA YA BWANA. Sala hii imebeba mambo mazito ambayo Mungu akitupa neema ya kuyapitia moja baada ya jingine Roho Mtakatifu atakusaidia kubadilika kwa kiwango kisichoneneka katika kuomba.
Mpendwa wangu kwa kujifunza somo hili nataka nikujengee ufahamu utakaokusaidia kuomba kwa Zaidi ya saa moja kila unapoingia katika maombi. Ujuzi huu kwa ujazo wa Roho Mtakatifu utasonga mbele na hakuna jambo gumu litakalosimama mbele yako utakaloshindwa kulisimamia katika maombi. Mpendwa wangu HAKUNA JAMBO LINASHINDIKANA KATIKA MAOMBI. Nimelithibitisha hilo. Ndo maana Bwana Yesu alithamini sana maombi. Hata Roho Mtakatifu asema kwa kinywa cha Paulo ‘“ombeni bila kukoma “1Thes 5:17
Pasipo kujali dhehebu lako nataka nikujengee msingi wa kuwa muombaji mwenye maarifa ya kiungu na nguvu za Roho Mtakatifu. Wengine wamekariri ili uwe mwombaji ni lazima ujiunge na dhehebu Fulani. Nakuhakikishia maadamu umemuamini Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako unayo nafasi ya kuwa mjuzi katika maombi kwani Roho Mtakatifu ndiye mwalimu wako. Sitaki ukariri mambo mpendwa wangu. Natamani ujifunze uwe na utaalamu binafsi na uzoefu wako binafsi na Mungu unayemtumikia jinsi atendavyo kazi katika maisha yako ya kila siku.
Labda nikuulize mpendwa wangu ni mara ngapi kwa siku tunaacha kula chakula??? Nadhani ni mara chache sana. Tena kuna wakristo wengine ukiwagusa kwenye suala la kuacha kula atakuona kama kichaa. Akigundua umefunga huli chakula kwa ajili ya maombi anakushangaa. Kwanini anashangaa, kwa sababu kula ni desturi ya kila siku ya mwanadamu. Kama ambavyo kila leo tunakula chakula hiki cha kimwili hadi tunakuwa na uzoefu wa vyakula tofauti tofauti je si Zaidi kujiwekea muda wa kuwa na maombi kila siku? Si vema mpendwa wangu ukajifunza kuomba kila siku kwa ajili ya kuutafuta uso wa Mungu maishani mwako? Au kwako haina maana yoyote kuwa karibu na Mungu katika maisha yako ya kila siku? Hutaki uongozi wa Mungu katika maisha yako binafsi ya kila siku? Hutaki uongozi wa Mungu katika masomo yako? Katika ndoa yako? Katika familia yenu? Katika jamii yenu? Katika kanisa lako? Katika Taifa lako? Huhitaji uongozi wa Mungu? Unataka nani akusaidie? Maana imeandikwa ‘Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata’  tena imeandikwa Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama’. Sasa Mungu atakufundishaje kama uko mbali naye hutaki kusema naye katika maombi?
Kuna njia 3 tutazifuata zitakazotusadia kuwa na maarifa na nguvu ya kuomba
1. Kujitengea muda maalumu wa kuomba (itakusaidia ujue muda gani wa kuomba na kuwa na muda wa mara kwa mara kuomba)
2. Kuwa na orodha ya maombi ya kuombea (itakusaidia ujue kila unapoingia kuomba nini unaenda kuombea)
3. Kuwa na mahusiano mazuri na Mungu (Mahusiano na Mungu yatakusaidia kutaka kila wakati kuwa karibu na Mungu katika maombi)
Kwa leo nikomee hapa na tukikutana tutaangalia mkakati wa 1 wa jinsi ya kuomba. Mungu akubariki. Ukiwa una jambo lolote unataka kutushirikisha tuombe pamoja nawe basi wasilian
0653543333
Baba lightnes

Jumanne, 14 Aprili 2015

Faith is capital

An aging King realized that if he died he has no one to take over the throne. He decided to adopt a son.

He launched a competition and 10 boys made it to the top. The King said to them, "I have one last test and whoever comes top will become my adopted son and heir to my throne".

He gave each boy a seed of corn and told them to take the seed home, plant and nurture it for 3 weeks. The 10 boys took their seeds and ran home to plant their seeds.

In one home, the boy and his parents were sad when the seed failed to sprout. The boy had done everything but he failed.

His friends advised him to buy a seed and plant it but his God fearing parents who had always taught him honesty refused.

The day came and the 10 boys went to the palace. All the 9 boys were successful.

The King went to each boy asking – “Is that what came out of the seed I gave you?" And each boy said "Yes, your majesty". The King would nod and move down the line until the last boy in the line who was shaking with fear.

The King asked him - "What did you do with the seed I gave you?" The boy said "I planted it and cared for it your majesty but it failed to sprout." The King went to the throne with the boy and said, "I gave these boys boiled seeds and a boiled seed cannot sprout.

If a King must have one quality, it must be honesty and only this boy passed the test.” We live in a society where people will do anything for success.

God sometimes does not give us things because He wants to teach us a lesson.

How many people out there have achieved success the wrong way? How many people send their children to expensive schools and build houses, buy expensive cars with stolen money?

How many people are occupying top positions yet they stole the certificates? How many people are successful out there at all costs?

HOW MANY PEOPLE WILL BE CROWNED AS KINGS IN HEAVEN FOR BEING FAITHFUL UNTIL THE END? I PRAY THAT I BE FAITHFUL TILL THE END!!!

Please be faithful to God no matter what life throws at you, even if life gives you boiled seed.

I hope you can spare me your precious time to send this to ten people to be faithful in their Christian life.

Kuzaliwa mara ya pili

KUZALIWA MARA YA PILI NI UHUSIANO WAKO BINAFSI NA MUNGU
Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.  Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye.  Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.  Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa? Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.  Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.  Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili. Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho.  Nikodemo akajibu, akamwambia, Yawezaje kuwa mambo haya? Yesu akajibu, akamwambia, Je! Wewe u mwalimu wa Israeli, na mambo haya huyafahamu? Amin, amin, nakuambia kwamba, Lile tulijualo twalinena, na lile tuliloliona twalishuhudia; wala ushuhuda wetu hamwukubali.  Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni?   Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.  Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa;  ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye #YOH 3:1-15
Mpendwa katika Kristo Yesu nakusalimu katika jina la Yesu. Ndugu yangu kuna watu wanadhani kuzaliwa mara ya pili ama kuokoka  ni kwa sababu ya kuabudu kwenye dhehebu Fulani labda na kufuata mapokeo Fulani Fulani. Kuna watu wanadhani kuwa mshirika wa dhehebu Fulani na kuwa kiongozi labda au kuwa mkuu wa kitengo Fulani katika kundi Fulani kanisani ni tiketi ya kuokoka. Bwana Yesu anasema ‘Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu’. Hapa duniani hata mbinguni. Kama kanisa linaweza kuwa na mtu ambaye anajiita tu Askofu, Mchungaji, Nabii, Mtume, Padri, Shemasi au Mwinjilisti kwa kujiita tu bila kuzaliwa mara ya pili hakika hatauona ufalme wa Mungu.
Nilikuwa nikiongea na Mchungaji mmoja juzi akanisimulia habari ya ‘Mwinjilisti’ mmoja ambaye alikuwa mchawi maeneo fulani! Nilimuuliza mara mbili mbili mtu mchawi halafu kapewa ‘title’ ya kuwa Mwinjilisti Kanisani??! Akanambia ndivyo ilivyokuwa. Yule mtu aliwekwa kazini kama Mwinjilisti. Kazi yake akabaki kuroga waumini na kuleta kila aina ya migogoro kanisani! Nilishangaa, nikalishangaa kanisa alilokuwa akitumika na nikawashangaa waumini aliokuwa akiwachunga!
Mpendwa wangu kuzaliwa mara ya pili hakika ni mahusiano ya mtu binafsi na Mungu. Mazungumzo ya Bwana Yesu na Nikodemo yatatufunulia hakika ya kwamba mwanadamu aliyezaliwa kwa asili ya kibinadamu anapaswa kuzaliwa kwa asili ya kimbingu ili aweze kuurithi ufalme wa Mungu. ‘Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho’!
Mwanadamu alivyoanguka pale Edeni alipungukiwa na utukufu wa Mungu kwa kuwa kabla ya anguko aliumbwa kwa taswira na mfano wa Mungu. Asipofanywa upya ndani ya moyo wake na maisha kwa ujumla hawezi kamwe kuurithi ufalme wa Mbinguni. Na anafanywa upya kwa kutubu dhambi zake na kumwamini Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yake naye aoshwe  dhambi zake na Roho Mtakatifu kwa damu ya Yesu na hivyo kuanza maisha mapya katika uhusiano wake na Roho Mtakatifu. Hili ni jambo la rohoni mpendwa lenye impact katika mwili. Sivyo kama wengine wanavyodhani. Wengine wanadhani ni kubatizwa kimwili. ‘Si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu #Tito 3:5. Kufanywa upya huku ndiko kunakoitwa ‘kuzaliwa mara ya pili’.
#Ezekiel 36:25-27 ‘Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi; nitawatakaseni na uchafu wenu wote, na vinyago vyenu vyote. Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.  Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda’
Kwanini kufanywa upya huku kuitwe kuzaliwa mara ya pili? Yamkini kama ambavyo kuzaliwa kwa kawaida kwa mwanadamu kulivyo, kwamba mtoto anapozaliwa, akianza kuivuta hewa hii duniani anatambulishwa na kuunganishwa na dunia hii. Ndivyo ilivyo na kuzaliwa kiroho kwamba tunatambulishwa na kuunganishwa katika ulimwengu wa Roho, tunaunganishwa maisha yetu na Roho na kuanza mahusiano na Mungu kwa roho zetu.
Kama ambavyo kuzaliwa kwa mwanadamu kimwili hufungua macho, masikio, na milango yote ya fahamu aweze kuona, kusikia, kuhisi n.k katika mambo yote ya kimwili vivyo hivyo tunapozaliwa katika roho tunafungua akili na fahamu zetu za rohoni tuone, tusikie na kuhisi vitu vya rohoni. Bwana Yesu anamuuliza Nikodemo ‘Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni (rohoni)? Paulo asema ‘Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu. Mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.  Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, TUKIYAFASIRI MAMBO YA ROHONI KWA MANENO YA ROHONI.  Basi MWANADAMU WA TABIA YA ASILI HAYAPOKEI MAMBO YA ROHO WA MUNGU; MAANA KWAKE HUYO NI UPUZI, WALA HAWEZI KUYAFAHAMU, KWA KUWA YATAMBULIKANA KWA JINSI YA ROHONI. Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu’.
Kuzaliwa kwa mwanadamu kimwili kunamleta duniani kufurahia kila kilicho chema katika dunia hii ambavyo kama asingezaliwa asingeweza kuvifurahia. Ndivyo ilivyo hata katika kuzaliwa katika roho tunaunganishwa na kufurahia maisha na vitu vya rohoni kama kufunuliwa kwa fahamu zetu kuijua kweli ya Mungu, kufanywa upya kwa mioyo yetu, kudhihirishwa kwa neema kuu ya wokovu wa Mungu kwetu, kupewa amani, furaha, upendo, kuwasiliana na Muumba Mungu Baba kwa njia ya Yesu Kristo na Roho Mtakatifu aishie ndani yetu.
Kuzaliwa kimwili kwa mwanadamu humtambulisha mtu kwa wanadamu wenziwe. Katika kuenenda katika maisha atashirikiana na wanadamu hawa katika mambo mbali mbali. Katika tamaa zao, hofu zao, huzuni zao, kazi n.k Ndivyo ilivyo na katika maisha ya rohoni tunatambulishwa kwa Wakristo wenzetu na katika kuenenda tunashirikiana nao katika mambo mbalimbali kama furaha zao katika kumtumikia Mungu, kufanywa upya kwa rohoni , upendo ,  amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu n.k.
Tunapozaliwa katika mwili tunaanza kujifunza kupokea, kujaribu kula vyakula vya kutusaidia kukua na kuishi hapa duniani, vivyo hivyo tunapozaliwa kwa jinsi ya rohoni tunaanza kujenga hamu na kushiriki kunywa maziwa ya akili yasiyoghoshiwa yaani neno la Mungu kwa watoto wote wa Yesu kisha tunaanza kula chakula kigumu kama ‘nyama’ inayofaa kwa ajili ya kukua katika kumtumikia Mungu. Naam hata kukua katika wokovu huu mkuu wa Mungu aliye Hai na kuwa na maarifa ya rohoni, na uzoefu na utakatifu hadi kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, yaani Kristo kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo.
Je mpendwa wangu hutamani kukua hadi kufikia cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo?

Mifungo

AINA YA MIFUNGO
Mpendwa wangu jana tuliangalia utangulizi wa kwanini tunafunga na aina ngapi za maombi. Leo tuziangalie hizo aina za mifungo na kwann tunafunga .
Kwanini tunafunga?
Kwa ujumla Tunafunga ili:
• Kuna watu wanafunga kwa sababu za kimwili kabisa. Kwamba miili yao imefika wakati inawapa shida. Matamanio ya mwili yameshindwa kuwasiliana vizuri na roho. Kuna nyakati tamaa za mwili zinakuwa kubwa na hivyo kwa kufunga na kuomba waweza kuutiisha mwili huu. Kwa vijana hasa, vyakula na vinywaji tunavyokula vinaleta shida wakati mwingine ndani ya mwili. Kwa kufunga unautiisha mwili na kuzinyamazisha tamaa hizo. Wengine wanafunga kwa ajili ya kuyatiisha mawazo. Bwana Yesu akasema mawazo ndiyo yamtiayo mtu unajisi. Kabla mtu hajafanya uasi Fulani huanza kujichafua katika mawazo yake. Ndani ya mawazo yake ataua, atamtukana mtu, atazini, ataiba yani atafanya kila lililo baya kabla hajalifanya katika ulimwengu wa kimwili. Rafiki yangu mmoja akasema ikiwa mwanadamu anaweza kupangilia mipango mbali mbali miovu hadi akaitimiza kwa nn asiweze kufanya hivyo hivyo kwa ajili ya Mungu? Kwa hyo wakati mwingine mtu anafunga kuyatiisha mawazo machafu ndani yake. Mawazo machafu hututia unajisi! Ndo maana mtume Paulo akasema “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu” 2Kor 7:1
• Lakini kiroho tunafunga ili kuweka mahusiano yetu na Mungu vizuri rohoni. Ezra 8:21-23
“Ndipo nikaamuru kufunga, hapo penye mto Ahava, ili tupate kujinyenyekeza mbele za Mungu, na kutafuta kwake njia iliyonyoka, kwa ajili yetu sisi wenyewe, na kwa ajili ya watoto wetu, na kwa mali yetu yote. Maana naliona haya kumwomba mfalme kikosi cha askari na wapanda farasi, ili kutusaidia juu ya adui njiani; kwa maana tulikuwa tumesema na mfalme, tukinena, Mkono wa Mungu u juu ya watu wote wamtafutao, kuwatendea mema; bali uweza wake na ghadhabu yake ni kinyume cha wote wamwachao.  Basi tukafunga, tukamsihi Mungu wetu kwa ajili ya hayo; naye akatutakabali”
Kiundani:
1. Kusudi kuu ni kuutafuta uso wa Mungu katika kile tunachokiomba 2Nyak 7:14
2. Kujinyenyekeza mbele za Mungu “Bali mimi, walipougua wao, Nguo yangu ilikuwa gunia. Nalijitesa nafsi yangu kwa kufunga; Maombi yangu yakarejea kifuani mwangu”- Zab. 35:13
3. Kupata usikivu toka kwa Mungu Isaya 58:9 “Ndipo utaita, na Bwana ataitika; utalia, naye atasema, Mimi hapa. Kama ukiiondoa nira; isiwepo kati yako, wala kunyosha kidole, wala kunena maovu”
4. Toba  kwa ajili ya mtu binafsi, Kanisa, au Taifa. Mfano: 1 Sam. 7:6 Nehemia 9:1-3
5. Maombolezo (Ezra 10:6) Daniel 10:2-3
6. Kutafuta ulinzi na uongozi wa Mungu katika mambo Fulani Fulani 2Nyak. 20:3 “Yehoshafati akaogopa, akauelekeza uso wake amtafute Bwana; akatangaza mbiu ya watu kufunga katika Yuda yote" waweza pia kuangalia Ezra 8:21-23 kama tulivyoona hapo juu. Mdo 14:23 “Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawaweka katika mikono ya Bwana waliyemwamini.” Neh 1:4 “hata ikawa niliposikia maneno hayo, nikaketi, nikalia, nikaomboleza siku kadha wa kadha; kisha nikafunga, nikaomba mbele za Mungu wa mbinguni”
7. Kama sehemu ya kumwabudu Mungu (Waamuzi 20:26, (Neh 9:1-3) (Luka 2:36-37)
8. Kwa ajili ya maombezi (Isaya 58:6-7, Daniel 6:18)
9. Kufanya ukombozi kwa ajili ya utumwa wa kiroho (Isaya 58:6, Mathayo 17:18-21)
10. Kujiandaa kwa ajili ya huduma maalumu (Mathayo 4:1-2, (Luka 4:1-2, Mdo 13:2-3
11. Kurudisha afya ya mtu (ISaya 58:8-11)
12.  Kuimarisha ndoa (1 Kor 7:5)
Aina ya mifungo:
1. Mfungo kamili
Katika mfungo huu hakuna kula kabisa chakula kigumu bali waweza kunywa maji au kimiminika chochote cha kukusupport.
Siku ngapi waweza kufunga mfungo wa aina hii unategemea na neema na malengo yako katika mfungo huo. Wengine huenda siku moja, mbili, tatu, wiki, n.k n.k
2. Mfungo nusu
Mfungo nusu huanzia saa 12 asbh hadi saa 9 mchana au kuanzia jua linapoibuka hadi linapozama. Mfungo ambao madhehebu mengine wamewazoeza waumini wao kuufanya. Wengine wameweza kuufanya kila ijumaa. Madhehebu ambayo yamewazoesha watu wao kufunga angalau kila wiki mara moja wameweza kuwa na mafanikio makubwa sana katika kuzifungua nira na vifungo mbali mbali
3. Mfungo wa Daniel
Daniel alifunga mifungo miwili ya aina yake;
• Katika Sura ya I Daniel alifunga alikula mboga mboga tu (Yaweza kuwa alikula mboga mboga na juisi Fulani Fulani)
• Katika sura ya 10 Daniel alifunga kwa siku 21  kwa kutokula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwake”
Tutaendelea na Mungu akubariki. Ukiwa una jambo lolote unataka kutushirikisha tuombe pamoja nawe basi wasiliana nami
0653543333
Andulileemanuel@gmail.com
Au soma katika blog
www.tukofarini.blogsport.com